DKT. MANDAI ARUDISHA FOMU YA KUWANIA NAFASI YA UBUNGE KIGAMBONI

 



Mmoja wa vijana waliojitokeza kuwania nafasi ya Ubunge katika Jimbo la Kigamboni, Dkt. Ally Mandai,  Julai 1, 2025, amerejesha rasmi fomu ya kuomba kuteuliwa kupeperusha bendera ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mkuu ujao.

 

Dkt. Mandai amewasili katika ofisi za CCM Wilaya ya Kigamboni mapema asubuhi baada ya kukamilisha taratibu zote za kikatiba na za chama zinazohitajika kwa wagombea wanaotaka kushiriki mchakato wa kuomba ridhaa ya chama hicho tawala.

 

Hatua ya kurejesha fomu inaashiria mwanzo rasmi wa safari ya Dkt. Mandai ndani ya mchakato wa kura za maoni za CCM kupitia jimbo la Kigamboni, ambao utatumika kumpata mgombea atakayepeperusha bendera ya chama hicho katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.

 

#KhomeinTvUpdates 

 

✍️Mwandishi wetu

 

PIA USIACHE KU SUBSCRIBE

CHANEL YETU Khomein TV

YOUTUBE UWE WA KWANZA 

KUFIKIWA NA HABARI ZETU

 

Follow Insta & Threads @khomeintv_

Tufollow pia kwenye X (Twitter), TikTok

@khomeintv na Facebook Khomein Tv

Post a Comment

0 Comments