AJALI YAUA WATU 9 ROMBO KILIMANJARO

 

Watu tisa wamefariki dunia kufuatia ajali iliyotokea mapema leo desemba 26,2024 Tarakea wilayani Rombo mkoa wa Kilimanjaro ikihusisha basi la abiria la kampuni ya Ngassero lililogongana uso kwa uso na gari  dogo la abiria aina ya Toyota Noah.

 

Kwa mujibu wa taarifa za mashuhuda kutoka eneo la ajali wameleza kuwa Basi la kampuni ya Ngassero linalofanya safari zake kati ya Tarakea na Dodoma lilikua likielekea Tarakea na gari dogo la abiria lilikua likitoka Tarakea kuelekea Moshi .

 


Mkuu wa wilaya ya Rombo Raymond Mangwala amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kwamba miili ya marehemu imehifadhiwa katika Hospitali ya Karume iliyopo wilayani humo huku dereva wa basi la Ngassero akidaiwa kukimbia .

 

“ Ni kweli kumetokea ajali mbaya iliyosababisha vifo vya abiria tisa Pamoja na dereva waliokuwa kwenye gari dogo , inaonekana dereva wa gari dogo alikua akiovertake gari jingine ndipo likakutana na basi  na Ngassero “ alisema Mangwala .

#KhomeinTvUpdates 

 

️ Mwandishi wetu

 

PIA USIACHE KU SUBSCRIBE

CHANEL YETU Khomein TV

YOUTUBE UWE WA KWANZA 

KUFIKIWA NA HABARI ZETU

 

Follow Insta & Threads @khomeintv_

Tufollow pia kwenye X (Twitter), TikTok

@khomeintv na Facebook Khomein Tv

Post a Comment

0 Comments