RAIS DKT. SAMIA ATENGUA HADHI YA UBALOZI KWA POLEPOLE

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ametengua uteuzi wa Hamphrey Polepole aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba na kumuondolea hadhi ya ubalozi.

 

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, kupitia Katibu Mkuu wake, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo imeeleza kwamba imepokea barua yenye taarifa hiyo kutoka kwa Katibu Mkuu Kiongozi, Dkt. Moses Kusiluka.

 

Kwa mujibu wa barua hiyo, uamuzi huo umeanza tangu Julai 16, 2025.

 

Aidha, Rais Dk. Samia, kwa mamlaka aliyonayo chini ya utumishi wa umma na kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, amemuachisha kazi Polepole kwa manufaa ya umma.

 

#KhomeinTvUpdates 

 

✍️Mwandishi wetu

 

PIA USIACHE KU SUBSCRIBE

CHANEL YETU Khomein TV

YOUTUBE UWE WA KWANZA 

KUFIKIWA NA HABARI ZETU

 

Follow Insta & Threads @khomeintv_

Tufollow pia kwenye X (Twitter), TikTok

@khomeintv na Facebook Khomein Tv

Post a Comment

0 Comments