SERIKALI YAAGIZA TAMRISO KUGAWA MIRABAHA 2025

 

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeielekeza Kampuni ya Kukusanya na Kugawa Mirabaha ya Tanzania Music Rights Society (TAMRISO), kuhakikisha wanafanya mgao wa mirabaha unaotarajiwa kufanyika mwanzoni mwa mwaka 2025 kwa makusanyo ya 2023/2024 na 2024/2025 (Julai hadi Disemba).

 

Maagizo hayo yametolewa na Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma ‘MwanaFA’, Jijini Dar es Salaam.

 

Kwa mujibu wa taarifa ya Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, Kampuni hiyo iliyoundwa na Wasanii wa Muziki, ndiyo yenye jukumu la kukusanya na kugawa mirabaha hiyo ya Wasanii.

 

#KhomeinTvUpdates

 

️ Mwandishi wetu

 

PIA USIACHE KU SUBSCRIBE

CHANEL YETU Khomein TV

YOUTUBE UWE WA KWANZA 

KUFIKIWA NA HABARI ZETU

 

Follow Insta & Threads @khomeintv_

Tufollow pia kwenye X (Twitter), TikTok

@khomeintv na Facebook Khomein Tv

Post a Comment

0 Comments