SERIKALI YATAKA UJENZI BRT UFANYIKE USIKU NA MCHANA

 

Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imejipanga kuwahudumia wananchi bila kuchoka kwa lengo la kuhakikisha hakuna kipingamizi katika kuyafikia maendeleo.

 

Katika kufanikisha hilo Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega amewataka wakandarasi wa ujenzi wa njia za mabasi yanayokwenda haraka, kuhakikisha wanafanya kazi usiku na mchana ili kuukamilisha mradi huo haraka.

 

Katika mwanzo wa ziara yake Mkoani Dar es salaam Waziri Ulega amekagua maendeleo ya mradi wa BRT 3 Lot 1 kuanzia Mtaa wa Azikiwe, Posta ya zamani hadi Gongolamboto pamoja na mradi wa uboreshaji usalama barabarani katika mradi wa BRT 1 sehemu A kutoka Ubungo hadi Kimara na kuzungumza na wananchi.

 

Akizungumza na Menejimenti ya TANROADS pamoja na wataalamu wengine wanaosimamia mradi huo, aliwataka kuhakikisha kazi haisimami na inakamilika kwa wakati, hivyo njia pekee ni kufanya kazi usiku na mchana.

 

#KhomeinTvUpdates 

 

✍️Mwandishi wetu

 

PIA USIACHE KU SUBSCRIBE

CHANEL YETU Khomein TV

YOUTUBE UWE WA KWANZA 

KUFIKIWA NA HABARI ZETU

 

Follow Insta & Threads @khomeintv_

Tufollow pia kwenye X (Twitter), TikTok

@khomeintv na Facebook Khomein Tv

Post a Comment

0 Comments