BREAKING: JOB NDUGAI AFARIKI DUNIA

 

Spika wa Bunge Mstaafu na aliyekuwa Mbunge wa Kongwa jijini Dodoma, Job Yustino Ndugai, amefariki dunia leo Agosti 06, 2025 jijini Dodoma.

 

Taarifa iliyotolewa na Kitengo cha Mawasiliano na Elimu kwa Umma cha Ofisi ya Bunge imesema “"Kwa masikitiko makubwa, naomba kutoa taarifa ya kito cha kiongozi

wetu, mwanasiasa mkongwe na Spika Mstaafu wa Bunge Mheshimiwa Job Yustino Ndugai kilichotokea leo jijini Dodoma. Natoa pole kwa familia ya Marehemu, ndugu, jamaa na Wananchi wa Jimbo la Kongwa, Mwenyezi Mungu awape moyo wa uvumilivu na subira katika kipindi hiki kigumu, amesema Mheshimiwa Spika.” Imeeleza taarifa hiyo, ikimnukuu Spika wa Bunge la Tanzania Dkt. Tulia Ackson.

 

Taarifa hiyo imesema Ofisi ya Bunge kwa kushirikiana na Kamati ya Mazishi pamoja na familia ya Marehemu inaratibu mipango ya mazishi na taarifa zaidi zitaendelea kutolewa. Mwenyezi Mungu ailaze Roho ya Marehemu Mahali Pema Peponi, Amina.

 

#KhomeinTvUpdates 

 

✍️Juma Mohamed

 

PIA USIACHE KU SUBSCRIBE

CHANEL YETU Khomein TV

YOUTUBE UWE WA KWANZA 

KUFIKIWA NA HABARI ZETU

 

Follow Insta & Threads @khomeintv_

Tufollow pia kwenye X (Twitter), TikTok

@khomeintv na Facebook Khomein Tv

Post a Comment

0 Comments