TANDAHIMBA WAKADIRIA KUKUSANYA ZAIDI YA BIL. 40.2 MWAKA WA FEDHA 2025/2026

 

Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba mkoani Mtwara, imekadiria kukusanya kiasi cha zaidi ya shilingi Bilioni 40.2, katika mwaka wa fedha ujao wa 2025/2026, ili kufanikisha utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

 


Hayo yameelezwa na Mkuu wa Idara ya Mipango na Uratibu wa Halmashauri hiyo, David Sinyanya, wakati akiwasilisha makadirio ya mpango wa Bajeti ya halmashauri hiyo katika kikao cha Baraza la Madiwani, kilichofanyika leo Februari 13, 2025, kikiongozwa na mwenyekiti Baisa Abdallah Baisa.

 


Amesema, katika makadirio hayo, fedha zilizokadiriwa kutokana na mapato ya ndani ya Halmashauri ni Bilioni 7.3.

 


Amesema fedha nyingine ni ruzuku ya mishahara ambayo ni Bilioni 24.9, matumizi mengineyo (OC) Bilioni 2.8 na ruzuku ya wafadhili ni Bilioni 5.065.

 

#KhomeinTvUpdates 

 

✍️Juma Mohamed-Tandahimba

 

PIA USIACHE KU SUBSCRIBE

CHANEL YETU Khomein TV

YOUTUBE UWE WA KWANZA 

KUFIKIWA NA HABARI ZETU

 

Follow Insta & Threads @khomeintv_

Tufollow pia kwenye X (Twitter), TikTok

@khomeintv na Facebook Khomein Tv

Post a Comment

0 Comments