MBUNGE NJEZA ATEMBELEA WAFIWA AJALI ILIYOUA 29 MLIMA IWAMBI

 


Mbunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini Oran M. Njeza, amezitembele na kutoa mkono wa pole kwa  familia za watu 29 waliofariki na majeruhi  wa ajali .

 

Ajali hiyo ilitokea  Juni 7,2025, katika mtelemko mkali wa mlima Iwambi Wilaya ya Mbeya ,  baada ya ya Lori lilokuwa limebeba shehena za unga kugonga  magari mawili yakiwepo ya abiria.

 

Katika ajali hiyo watu 28 walipoteza maisha papo hapo na wengine tisa kujeruhiwa na kukimbizwa katika Hosptali Teule ya Ifisi Wilaya ya Mbeya.

 

Mbunge Njeza ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bajeti ya Bunge, licha ya kutoa pole amezitaka familia za majeruhi kuendelea kuwaombea.

 

Amesema baada ya  kuwasilisha hoja za kamati bungeni jijini  Dodoma Juni 16, 2025 ,amelazimika kurejea jimboni kutoa mkono wa pole kwa  familia zilizo poteza wapendwa wao na kuwajulia hali  majeruhi wote wa ajali hiyo.

 

"Nilipokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya ajali hiyo  mbaya ,lakini pia nipongeze serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan  kwa kujitoa  kushirikiana na familia za wafiwa na majeruhi.

 

#KhomeinTvUpdates 

 

✍️Mwandishi wetu-Mbeya

 

PIA USIACHE KU SUBSCRIBE

CHANEL YETU Khomein TV

YOUTUBE UWE WA KWANZA 

KUFIKIWA NA HABARI ZETU

 

Follow Insta & Threads @khomeintv_

Tufollow pia kwenye X (Twitter), TikTok

@khomeintv na Facebook Khomein Tv


Post a Comment

0 Comments