SERIKALI YAWATAKA WATANZANIA KUENDELEA KUUTUNZA UPENDO, UMOJA NA AMANI

 

Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, imetoa wito kwa Watanzania kuendelea  kulinda amani, upendo,umoja na mshikamano wetu kwa maslahi ya taifa.

 

Wito huo umetolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa wakati alipoungana na waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Kiruruma katika Ibada ya Krismasi, Disemba 25,2024

 

“Tukipendana tutakuwa wamoja, tutakuwa na amani, lakini kuna tunu nyingine ya ujirani mwema na kufanya matendo ya huruma” amesema Bashungwa

 

Bashungwa amesema kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na taasisi za kidini likiwemo Kanisa Katoliki ambalo ni miongoni mwa  Makanisa yenye mchango mkubwa katika kuwakumbusha Watanzania kuishi kwa upendo na amani.

 

“Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan itaendelea kushirikia na taasisi za dini likiwemo Kanisa letu Katoliki kwa kuwa ni miongoni mwa makanisa yanafundisha Watanzania kuwa raia wema” amesisitiza Bashungwa

 

Awali, Paroko Msaidizi wa Parokia ya Kiruruma, Padre Salapioni Mberwa amewaasa Waumini wa Kanisa Katoliki kuiadhimisha Sikukuu ya Krismasi kwa kukumbuka upendo wa Mwenyezi Mungu kwa Wanadamu.

 

#KhomeinTvUpdates 

 

️Mwandishi wetu

 

PIA USIACHE KU SUBSCRIBE

CHANEL YETU Khomein TV

YOUTUBE UWE WA KWANZA 

KUFIKIWA NA HABARI ZETU

 

Follow Insta & Threads @khomeintv_

Tufollow pia kwenye X (Twitter), TikTok

@khomeintv na Facebook Khomein Tv

Post a Comment

0 Comments