TULIA TRUST YAPANDA MITI 500 KUTUNZA MAZINGIRA

Taasisi ya Tulia Trust inayojihusisha na kuwezesha wananchi kiuchumi na misaada kwa jamii imepanda miti zaidi ya 500 katika Kata tisa  jijini Mbeya kwa  lengo la kuhamasisha  utunzaji  mazingira na kurejesha uoto wa asili.

 

Kampeni hiyo  endelevu ambayo imeanza rasmi jana Ijumaa Januari 14,2025 ikiongonzwa na Ofisa Habari na  Mawasiliano wa Taasisi ya Tulia Trust , Joshua Mwakanolo.

 


Mwakanolo ameongoza zoezi hilo  kwa niaba ya Mkurugenzi wa Taasisi hiyo ambaye ni Spika wa Bunge, Mbunge wa Mbeya mjini na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) Dkt Tulia Ackson.

 

Amesema lengo la kampeni  hiyo ni  kuhamasisha jamii hususani mashuleni utunzaji mazingira kwa kupanda miti rafiki inayo himili mabadiliko ya tabia nchi.

 

Ametaja maeneo yaliyopandwa miti ni Kata za  Iganjo, Iduda, Uyole, Igawilo, Nsalaga, Itezi, Isyesye, Ruanda na Sinde ambapo kila kata imepandwa miti 56 ya kivuli na matunda.

 


Amesema kampeni hiyo ni endelevu na itazifikia  kata  zote  36 za  Jiji la Mbeya  kwa kupanda miti ya matunda na vivuli na hii ni awamu ya pili huku lengo ni kupanda miti 2000.

 

Mkazi wa Nsalaga Seleman Juma amesema kampeni hiyo iendane na kutoa elimu kwa jamii kuelewa umuhimu wa kutunza mazingira kwa kupanda miti na kutunza rasirimali hiyo.

 

#KhomeinTvUpdates 

 

✍️ Mwandishi wetu-Mbeya

 

PIA USIACHE KU SUBSCRIBE

CHANEL YETU Khomein TV

YOUTUBE UWE WA KWANZA 

KUFIKIWA NA HABARI ZETU

 

Follow Insta & Threads @khomeintv_

Tufollow pia kwenye X (Twitter), TikTok

@khomeintv na Facebook Khomein Tv

 



Post a Comment

0 Comments