WAGOMBEA SITA WAPITISHWA KUWANIA USPIKA WA BUNGE

 

Jumla ya wagombea Sita wa kiti cha Uspika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka vyama Sita vya Siasa wamepitishwa na Ofisi ya Katibu wa Bunge na Msimamizi wa uchaguzi kuwania kiti hicho.

 

Taarifa iliyotolewa na Katibu wa Bunge na Msimamizi wa Uchaguzi huo Baraka Leonard, imesema wagombea waliopitishwa ni Mussa Azzan Zungu kutoka Chama cha Mapinduzi (CCM), Veronica Charles Tyeah kutoka Chama cha National Reconstruction Alliance (NRA), Anitha Alfan Maya kutoka Chama cha National League for Democracy (NLD), Chrisant Nyakitita kutoka Chama cha Democratic Party

(DP), Ndonge Said Ndonge kutoka Chama cha Alliance for

Africa Farms Party (AAFP) na Amin Alfred Yango kutoka Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC).

 

“Hivyo, bila kuathiri Shughuli nyingine zitakazopangwa na Bunge,

tarehe 11 Novemba, 2025 saa Tatu asubuhi au muda mfupi baada ya hapo, nitawasilisha majina ya Wagombea walioteuliwa kwa Wapiga kura ambao ni Wabunge Wateule wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili Uchaguzi ufanyike kwa mujibu wa utaratibu utakaotolewa wakati wa Uchaguzi.” Imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.

 

#KhomeinTvUpdates 

 

✍️Juma Mohamed

 

PIA USIACHE KU SUBSCRIBE

CHANEL YETU Khomein TV

YOUTUBE UWE WA KWANZA 

KUFIKIWA NA HABARI ZETU

 

Follow Insta & Threads @khomeintv_

Tufollow pia kwenye X (Twitter), TikTok

@khomeintv na Facebook Khomein Tv

Post a Comment

0 Comments