SERIKALI KUJA NA MKAKATI WA KUSHUSHA BEI YA DAWA, VIFAA TIBA

 

Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Godwin Mollel, Februari 18, 2025, amefanya majadiliano na Bodi ya Ushauri pamoja na Menejimenti ya Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) kuhusu mikakati bora ya kukabiliana na bei kubwa za dawa nchini. 

 

Katika majadiliano hayo, Dkt. Mollel ameainisha changamoto ya kuwepo kwa hali ya soko ambalo linadhibitiwa na watu wachache (monopoly), hali inayosababisha bei za dawa kuwa kubwa na kuongeza gharama za tiba kwa wananchi.

 

Dkt. Mollel amebainisha kuwa, kwa kuanzisha ushindani katika soko la dawa na vifaa tiba, bei hizo zitaweza kushuka, na hivyo kuboresha upatikanaji wa huduma za afya. 

 

Ameongeza kuwa, mpango huo utasaidia kuimarisha Mfuko wa Bima ya Afya kwa Wote, na kuongeza upatikanaji wa huduma bora kwa wananchi.

 

#KhomeinTvUpdates 

 

✍️Mwandishi wetu

 

PIA USIACHE KU SUBSCRIBE

CHANEL YETU Khomein TV

YOUTUBE UWE WA KWANZA 

KUFIKIWA NA HABARI ZETU

 

Follow Insta & Threads @khomeintv_

Tufollow pia kwenye X (Twitter), TikTok

@khomeintv na Facebook Khomein Tv

Post a Comment

0 Comments