SERIKALI YAENDELEA KUWANOA WATENDAJI WAKE KUHUSU MFUMO WA NeST

 

Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia Ofisi ya Rais TAMISEMI imeendelea na jitihada zake kuhakikisha watendaji wake wanapata ujuzi wa matumizi ya mifumo mbalimbali ukiwemo mfumo wa NeSt.

 

Kupitia dhamira hiyo, Tamisemi wameanza kutoa Mafunzo ya Mfumo wa NeST, ambapo awamu ya kwanza imeanza Februari 04, 2025 katika Ukumbi wa Mabeyo jijini Dodoma

 

Aidha, Mafunzo hayo yatahudhuriwa na  Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa, Makatibu Tawala Wasaidizi wa Miundombinu na Maafisa Manunuzi kutoka Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa ambao ndio walengwa wakuu.

 

Mgeni rasmi katika mafunzo hayo anatarajiwa kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mohammed Mchengerwa, viongozi wengine ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-TAMISEMI Sospeter Mtwale sambamba na Mkurugenzi Mkuu wa PPRA Bw. Denis K. Simba.

 

#KhomeinTvUpdates 

 

✍️Mwandishi wetu

 

PIA USIACHE KU SUBSCRIBE

CHANEL YETU Khomein TV

YOUTUBE UWE WA KWANZA 

KUFIKIWA NA HABARI ZETU

 

Follow Insta & Threads @khomeintv_

Tufollow pia kwenye X (Twitter), TikTok

@khomeintv na Facebook Khomein Tv

Post a Comment

0 Comments