Kamati ya kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI chini ya Mwenyekiti wake Elibarick Kingu imeitaka Serikali kupitia Wizara ya Afya kuimarisha huduma za afya ya akili na kuhakikisha vituo vyote vya kutolea huduma za afya nchini vinawezeshwa kutoa huduma za msingi za afya ya akili.
Hayo yamesemwa Februari 4, 2025 na Mwenyekiti huyo wakati akiwasilisha taarifa ya Kamati mbele ya Bunge la 12 la Mkutano wa 18, kikao cha sita.
Kingu amesema kumekuwa na ongezeko kubwa la matatizo ya afya ya akili nchini hali iliyosababisha jamii kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi na kupungua kwa uwezo wa kuzalisha mali, hivyo ameitaka Serikali kuhakikisha elimu ya afya ya akili inatolewa kwa jamii pamoja na kuongeza wataalam wa kutoa huduma za afya ya akili.
Ameongeza kuwa, kamati hiyo inapendekeza Serikali kurejesha kwa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA), udhibiti wa chakula na vipodozi kutoka Shirika la Viwango Tanzania (TBS), kwani bidhaa za chakula na vipodozi zinahusiana moja kwa moja na afya ya jamii.
✍️Mwandishi wetu
PIA USIACHE KU SUBSCRIBE
CHANEL YETU Khomein TV
YOUTUBE UWE WA KWANZA
KUFIKIWA NA HABARI ZETU
Follow Insta & Threads @khomeintv_
Tufollow pia kwenye X (Twitter), TikTok
@khomeintv na Facebook Khomein Tv
0 Comments