SERIKALI YAZIDI KUUTANGAZA UTALII NJE YA NCHI


 Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuutangaza utalii katika Mkutano wa Utalii na Uwekezaji unaoendelea katika ukumbi wa Eros Hotel, Nehru Place, Delhi, India.

 

Tanzania imeshiriki mkutano huo kwa kupitia Kituo cha Uwekezaji (TIC) ambacho kimetoa wasilisho kuhusu fursa za uwekezaji zilizopo nchini Tanzania na kutoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali yanayohusu uwekezaji wakati wa mikutano ya biashara ya ana kwa ana (B2B) sambamba na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB).

 

Msafara wa Tanzania umeongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Mh. Nkoba Mabula. Wengine ni Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Bw. Ephraim Mafuru, Wajumbe wa Bodi pamoja na wawakilishi wa taasisi mbalimbali za Serikali, ikiwemo TIC.

 

Mgeni rasmi wa hafla hiyo ni Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Anisa Mbega. 

 

#KhomeinTvUpdates 

 

✍️Mwandishi wetu

 

PIA USIACHE KU SUBSCRIBE

CHANEL YETU Khomein TV

YOUTUBE UWE WA KWANZA 

KUFIKIWA NA HABARI ZETU

 

Follow Insta & Threads @khomeintv_

Tufollow pia kwenye X (Twitter), TikTok

@khomeintv na Facebook Khomein Tv



Post a Comment

0 Comments