Baraza la Michezo la Taifa, limetambua na kuthamini juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika tuzo za wanamichezo waliofanya vizuri katika mashindano ya Kimataifa zinazoandaliwa na Baraza hilo.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amemwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika hafla hiyo na kupokea tuzo ya kutambua mchango wa Rais Samia katika kukuza na kuendeleza sekta ya michezo nchini, hafla ambayo imefanyika katika ukumbi wa Super dome Masaki jijini Dar es Salaam Juni 01, 2025.
Lengo la tuzo hizo ni kuwaenzi na kuwatambua Watanzania wanaoiwakilisha nchi katika michezo mbalimbali duniani na kuiletea sifa Tanzania kwa maslahi yao na Taifa kwa ujumla.
Akizungumza Katika hafla hiyo, Waziri Mkuu amesema kuwa Serikali ya awamu ya Sita itaendelea kuwekeza katika sekta ya michezo kwa kuwa inatambua michezo ni afya, ajira, mshikamano, maendeleo lakini pia michezo ni burudani.
Aidha, Majaliwa pia amekabidhiwa tuzo ya kutambua mchango wake katika kusimamia michezo nchini.
#KhomeinTvUpdates
✍️Mwandishi wetu
PIA USIACHE KU SUBSCRIBE
CHANEL YETU Khomein TV
YOUTUBE UWE WA KWANZA
KUFIKIWA NA HABARI ZETU
Follow Insta & Threads @khomeintv_
Tufollow pia kwenye X (Twitter), TikTok
@khomeintv na Facebook Khomein Tv
0 Comments