Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limeibuka kinara na kukabidhiwa tuzo ya uhifadhi wa mazingira katika kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Mazingira Kitaifa yaliyofanyika Juni 05, 2025 jijini Dodoma. Ikiwa ni moja ya shirika linaloitendea haki ajenda ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, juu ya utunzaji wa mazingira
TANESCO imetunukiwa tuzo hiyo kutokana na kutambua mchango katika kuhifadhi mazingira kupitia utekelezaji wa miradi mbalimbali ikiwemo Mradi wa Kufua Umeme wa Julius Nyerere (JNHPP), ambao umeendelea kuzingatia misingi ya utunzaji wa mazingira sambamba na kuchangia kupunguza gesi joto nchini.
Tuzo hiyo ilitolewa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango, na kupokelewa na Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, katika hafla ya kufunga rasmi maadhimisho hayo.
Kwa kuzingatia umuhimu mazingira nchini, TANESCO kupitia ushiriki wake katika maonesho hayo, imedhamiria kuendelea kutekeleza miradi mikubwa ya umeme kwa kuzingatia usalama wa mazingira, ikiwa ni pamoja na JNHPP na mingine inayolenga kuleta manufaa kwa vizazi vya sasa na vijavyo.
#KhomeinTvUpdates
✍️Mwandishi wetu
PIA USIACHE KU SUBSCRIBE
CHANEL YETU Khomein TV
YOUTUBE UWE WA KWANZA
KUFIKIWA NA HABARI ZETU
Follow Insta & Threads @khomeintv_
Tufollow pia kwenye X (Twitter), TikTok
@khomeintv na Facebook Khomein Tv
0 Comments