MZRH KUFANYA UCHUNGUZI WA SARATANI BURE KWA WANANCHI

 

Hosptali ya Rufaa Kanda ya Mbeya (MZRH) inatarajia kutoa bure  huduma za  uchunguzi wa magonjwa ya saratani ikiwemo  tezi dume, shingo ya kizazi, matiti na mfumo wa chakula.

 

Akizungumza na waandishi wa habari leo Ijumaa, Januari 30, 2025 Daktari Bingwa wa Saratani Dkt. Tibera Rugumbwa amesema huduma hizo zitatolewa Februri 4 mwaka huu ikiwa ni siku ya maadhimisho ya saratani duniani.

 

Amesema lengo la kutoa huduma bure ni kusaidia wananchi  kufanyiwa vipimo vya uchunguzi ili kubaini kama wana saratani wapatiwe matibabu.

 

"Kwa Tanzania kati ya watu 45,000 wakifanyiawa uchunguzi nusu yake hupoteza maisha kutokana na tatizo la saratani kwa wanawake na wanaume ,"amesema.

 

Ametaja  saratani zinazo sababisha vifo kwa  mgonjwa akichelewa kupata matibabu ni pamoja na tezi dume, saratani ya shingo ya kizazi, matiti na mfumo wa chakula ambazo  hugundulika haraka.

 

Jesca John ameomba elimu zaidi kuendelea kutolewa kufuatia idadi kubwa kujifungia majumbani kutumia tiba za asili.

 

#KhomeinTvUpdates 

 

✍️ Mwandishi wetu-Mbeya

 

PIA USIACHE KU SUBSCRIBE

CHANEL YETU Khomein TV

YOUTUBE UWE WA KWANZA 

KUFIKIWA NA HABARI ZETU

 

Follow Insta & Threads @khomeintv_

Tufollow pia kwenye X (Twitter), TikTok

@khomeintv na Facebook Khomein Tv

Post a Comment

0 Comments