MIRADI YA ZAIDI YA MIL 253 YABAINIKA KUWA NA DOSARI MTWARA

 

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Mtwara imebaini mapungufu katika miradi nane yenye thamani ya shilingi 253,300,000.00 kati ya miradi 28 ya maendeleo katika sekta ya Elimu, Miundombinu pamoja na Afya.

 

Hayo yamesemwa leo january 31/2025 na  Mkuu wa Takukuru mkoa wa Mtwara  Elisante Mashauri ,wakati anazungumza na waandishi wa habari  kwenye ofisi za TAKUKURU ambapo amesema kuwa wamefungua kesi 9 ambazo zinaendelea Mahakamani, ambapo katika kesi hizo, jamhuri imeshinda kesi Moja.

 

“katika kipindi cha Januari hadi Machi tutaendelea kuhakikisha kwamba tunazuai vitendo vya rushwa na ubadhirifu katika makusanyo ya mapato kwenye  halmashauri ,tutakagua miradi ya maendeleo ili kuhakikisha kuwa thamani ya fedha inapatikana.”amesema Mashauri.

 

Aidha Mashauri  ametoa wito kwa wananchi  na wadau wote kuendelea kushirikiana katika kipindi cha uchaguzi wa viongozi utakaofanyika mwzi Oktoba mwaka huu ili kupata viongozi wasiojihusisha na vitendo vya rushwa kwa maendeleo ya Mtwara na Taifa kwa Ujumla.

 

"TAKUKURU Mkoa wa Mtwara tunawapongeza na kuwashukuru wananchi pamoja na watu  wote Kwa ushirikiano, tunapoelekea katika kipindi cha uchaguzi wa viongozi 2025 tuendelee kushirikiana ili kupata viongozi bora wasiojihusisha na vitendo vya rushwa” amesema Mashauri.

 

#KhomeinTvUpdates 

 

✍️ Ramla Masali-Mtwara

 

PIA USIACHE KU SUBSCRIBE

CHANEL YETU Khomein TV

YOUTUBE UWE WA KWANZA 

KUFIKIWA NA HABARI ZETU

 

Follow Insta & Threads @khomeintv_

Tufollow pia kwenye X (Twitter), TikTok

@khomeintv na Facebook Khomein Tv

Post a Comment

0 Comments