Polisi Mkoa wa Mbeya imesema limewatia nguvuni wafanyabishara wawili kwa makosa ya kuhujumu miundombinu ya Umeme na Maji.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Benjamin Kuzaga amesema watuhumiwa hao walikamatwa kwa nyakati tofauti katika eneo la Block T na Nzovwe jijini hapa.
Amewataja watuhumiwa hao kuwa ni mfanyabiashara wa vifaa vya umeme,Joseph Movin (53) na Rehema Jamson (42) mfanyabiashara wa vyuma chakavu.
Kuzaga amesema watuhumiwa hao wametiwa nguvuni baada ya kufanyika msako wa kushtukiza katika maeneo yao ya biashara na stoo za kuhifadhia vifaa.
Amefafanua kuwa katika msako huo Jeshi la Polisi lilishirikiana na maofisa wa Shirika la Umeme nchini (Tanesco) mikoa ya Nyanda za Juu Kusini na wataalam wa Mamlaka ya Maji Mbeya.
Amesema msako huo ni endelevu umefanywa kufuatia kuibuka kwa watu wasio wema kuhujumu miundombinu ya Taasisi za kiserikali hususani vifaa vya Transfoma, nyaya za copper na vifaa vya Maji
✍️ Mwandishi wetu-Mbeya
PIA USIACHE KU SUBSCRIBE
CHANEL YETU Khomein TV
YOUTUBE UWE WA KWANZA
KUFIKIWA NA HABARI ZETU
Follow Insta & Threads @khomeintv_
Tufollow pia kwenye X (Twitter), TikTok
@khomeintv na Facebook Khomein Tv
0 Comments