Zaidi ya watu 20, 000 wakiwemo wanafunzi wa Shule mbili za Sekondari Jijini Mbeya watanufaika na programu ya kidigali kwa wote itakayo tumia nishati ya umeme wa jua kupitia darasa linalotembea (Digitruck) kwa kushirikiana na Taasisi ya Tulia Trust.
Katibu Tawala Wilaya ya Mbeya, Mohammed Fakii amesema leo Jumanne Februari 11,2025 kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Beno Malisa wakati akizindua programu elimu ya kidigitali kupitia darasa linalotembea(Digitruck) chini ya mpango wa TECH 4 ALL wa Huawei ambao kwa Tanzania umeanza katika Mkoa wa Mbeya.
Fakii amesema kuwa ujio wa programu hiyo itawaongezea ujuzi kwa walimu wa masomo ya tehama na vijana kutafuta fursa mbalimbali za kiuchumi kwa kutumia mifumo ya kiditali.
"Kama tulivyo msikia mwakilishi wa Mkurugenzi wa Digitruck kuwa matarajio ni kuwafikia watu 20,000 kutokana na umuhimu wa matumizi ya teknolojia kwa sasa nilitamani watu 40,000 wafikiwe na programu hiyo,"amesema.
Amesema kwa nchi ya Tanzania ilichelewa kuanza programu na kwamba ni wakati sasa wananchi kuchangamkia fursa hiyo ambayo inakwenda kufungua wigo mpaka wa fursa za kibiashara na kiuchumi .
Fakii amesema programu hiyo ni matunda ya Mbunge wa Mbeya mjini, Dkt Tulia Ackson baada ya kufanya ziara nchini China na kutoa ombi lake la kutaka elimu ya Tehama ifike nchini Tanzania hususani kwa Mkoa wa Mbeya.
Akizungumza kwa njia ya mtandao Spika wa Bunge na Mbunge Mbeya mjini, Dkt Tulia Ackson amesema kwa Tanzania hii awamu ya kwanza na kuzinduliwa kwa Mkoa wa Mbeya katika shule ya sekondari Forest.
Amewataka wananchi kutumia fursa hiyo katika shughuli za kiuchumi, ujasiriamali na ujuzi kwa vijana katika matumizi ya mifumo ya tehama.
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Programu ya Digitruck,Bruce Zhao amesema lengo ni kuimarisha ujuzi wa kidigitali kwa vijana na wanawake huku akibainisha ni kuonyesha mashirikiano baina yao na Taasisi ya Tulia Trust ambayo Mkurugenzi wake Spika wa Bunge, Mbunge wa Mbeya mjini Dkt. Tulia Ackson.
"Tunatazama ushirikiano zaidi ili kufanikisha kauli mbiu "In Tanzania, For Tanzania" tunaamini kwa kushirikiana tutafanikisha mambo makubwa kwa mustakabali mzuri wa watanzania wote."amesema.
Baadhi ya wanafunzi wa shule zitakazo nufaika na programu hiyo wamemshukuru Mbunge wa Mbeya mjini ,Dkt Tulia Ackson kwa kuleta mfumo wa tehama kupitia darasa linalotembea ambalo litakuwa mwarobaini kwao kwenda na teknolojia ya kisasa ya kidigitali.
✍️Mwandishi wetu-Mbeya
PIA USIACHE KU SUBSCRIBE
CHANEL YETU Khomein TV
YOUTUBE UWE WA KWANZA
KUFIKIWA NA HABARI ZETU
Follow Insta & Threads @khomeintv_
Tufollow pia kwenye X (Twitter), TikTok
@khomeintv na Facebook Khomein Tv
0 Comments