NDINGO AGAWA MITUNGI YA GESI KWA MAMA LISHE AKIADHIMISHA MIAKA 48 YA CCM

 

Mbunge wa Jimbo la  Mbarali Mkoa wa Mbeya, Bahati Ndingo amegawa mitungi ya nishati ya safi ya gesi kwa Mama lishe 100 kutoka maeneo mbalimbali wilayani humo.

 


Ndingo amekabidhi  mitungi hiyo, Februari Mosi, baada ya kuwa Mgeni Rasmi katika Maadhimisho ya miaka 48 ya kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) yaliyo andaliwa na Jumuiya ya Umoja wa Wanawake (UWT) .

 


Ndingo amesema lengo la kutoa  nishati  hiyo ni kuunga mkono juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan,  katika  kuhamasisha wananchi kutunza mazingira na kugeukia matumizi ya nishati safi ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

 

Katika hatua nyingine, Ndingo kwa  kushirikiana na wajumbe wa Umoja wa wanawake UWT,  wametoa misaada mbalimbali kwa wanafunzi 27 wenye mahitaji maalumu katika Shule ya Msingi  Igomelo .

 


Pia wametoa mahitaji mengine yakiwemo mashuka, sabuni, mafuta na vifaa vya kuwasitili watoto kwenye Wodi ya  Wazazi  Hosptali ya Wilaya katika kuhitimisha maadhimisho ya kuzaliwa kwa CCM wilayani humo.

 

Ndingo amesema kampeni ya ugawaji nishati ya gesi ni endelevu lengo ni kuona jamii inaachana na matumizi ya kuni na mkaa ambayo sio salama kwa afya zao.

 


Baadhi ya Mama lishe wameshumshukuru Mbunge huyo kwa hatua ya kuwagusa kwani anakwenda kuokoa afya ya watu wengi ambao wamekuwa wakipata madhara kutokana na matumizi ya mkaa na kuni.

 

#KhomeinTvUpdates 

 

✍️ Mwandishi wetu-Mbeya

 

PIA USIACHE KU SUBSCRIBE

CHANEL YETU Khomein TV

YOUTUBE UWE WA KWANZA 

KUFIKIWA NA HABARI ZETU

 

Follow Insta & Threads @khomeintv_

Tufollow pia kwenye X (Twitter), TikTok

@khomeintv na Facebook Khomein Tv

Post a Comment

0 Comments