Kamati mpya ya Ukaguzi ya Wizara ya Nishati imefanya ziara katika miradi ya umeme mkoani Pwani ili kujionea utekelezaji wa miradi hiyo ili kuweza kumshauri vyema Katibu Mkuu Wizara ya Nishati juu ya usimamizi wa rasilimali za Wizara ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa miradi.
Ziara hiyo imefanyika katika Mradi wa kuzalisha umeme wa Julius Nyerere (JNHPP) na Kituo cha kupoza na kusambaza umeme cha Chalinze mkoani Pwani Mei 19 na 20, 2025
Baada ya kujionea utekelezaji wa miradi hiyo ambayo imekamilika, Mwenyekiti wa Kamati, Mhandisi Kenneth Nindie ameipongeza Serikali kwa kazi Kubwa inayofanya kwa maslahi mapana ya wananchi na Taifa kwa ujumla.
Amebainisha kuwa, Serikali ya Awamu ya Sita imewekeza fedha nyingi katika miradi ya umeme, hivyo Wizara ya Nishati wajibu wake ni kufanya usimamizi mzuri wa miradi ili thamani ya fedha ionekane.
Aidha, Kamati hiyo imewataka wakandarasi wanaopewa kazi ya kutekeleza miradi kuwa wazalendo kwa kuzingatia viwango na ubora ili miradi inayofanyika idumu kwa muda mrefu na kuleta matokeo chanya kwa Watanzania.
"Tunaipongeza Serikali kwa kweli inafanya kazi kubwa ya kutekeleza miradi mikubwa katika nchi yetu kwa manufaa mapana ya wananchi, kikubwa tunawasihi wakandarasi kuwa wazalendo katika kutekeleza majukumu yao, mikataba iliyowekwa izingatiwe kwa kutekeleza kazi kwa viwango na ubora ili miradi hii iwe na tija kwa Taifa." Amesema Nindie.
#KhomeinTvUpdates
✍️Mwandishi wetu
PIA USIACHE KU SUBSCRIBE
CHANEL YETU Khomein TV
YOUTUBE UWE WA KWANZA
KUFIKIWA NA HABARI ZETU
Follow Insta & Threads @khomeintv_
Tufollow pia kwenye X (Twitter), TikTok
@khomeintv na Facebook Khomein Tv
0 Comments