PROF. JANABI ASHINDA MKURUGENZI WHO AFRIKA

 

Mshauri wa Masuala ya Afya na Tiba wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Profesa Mohamed Janabi, amechaguliwa kuwa Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Kada ya Afrika.

 

Profesa Janabi, ameshinda kinyang’anyiro hicho katika uchaguzi uliofanyika leo Mei 18, 2025 jijini Geneva nchini Uswis, kuziba nafasi ilioachwa na aliyekuwa mkurugenzi mteule wa shirika hilo Dkt. Faustine Ndungulile, ambaye alifariki duniani siku chache baada ya kutangazwa mmshindi wa nafasi hiyo.

 

Prof. Janabi amewashinda Dk. N’da Konan Michel Yao wa Ivory Coast, Dk. Boureima Hama Sambo wa Niger, Dk. Drame Mohammed Lamine wa Guinea na Prof. Mijiyawa Moustafa wa Togo.

 

#KhomeinTvUpdates 

 

✍️Juma Mohamed

 

PIA USIACHE KU SUBSCRIBE

CHANEL YETU Khomein TV

YOUTUBE UWE WA KWANZA 

KUFIKIWA NA HABARI ZETU

 

Follow Insta & Threads @khomeintv_

Tufollow pia kwenye X (Twitter), TikTok

@khomeintv na Facebook Khomein Tv

Post a Comment

0 Comments