DKT TULIA KUSOMESHA WATOTO WAWILI WASIO JIWEZA

 

Kijana Nature Willson (18) Mkazi wa Mtaa wa Mwasote Kata ya Itezi Jiji la Mbeya aliyekwama kujiunga kidato cha tano kutokana na ukata wa fedha amefutwa machozi na Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson baada ya kubeba jukumu la kuwatunza na  kuwasomesha yeye na mdogo wake Patrick Willson (8).

 

Nature    amehitimu kidato cha nne  Sekondari Itezi  jijini hapa na kuchaguliwa kujiunga kidato cha tano  katika Shule ya  Sekondari ya Wavulana ya  Rungwe baada ya kupata ufauru wa  daraja la kwanza na pointi 13 , huku wakiishi  mazingira magumu na kulelewa  na bibi yao Lucia Kapangali (65) ambaye ajiwezi kiuchumi.

 


Uamuzi wa Dkt. Tulia ambaye pia ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), kuchukua jukumu la kuitunza na  kuisomesha familia hiyo   

  ni baada ya  kuibuliwa na mbio za bendera ya upendo iliyokimbizwa hivi karibuni kupitia Taasisi yake ya Tulia Trust.

 

Bendera hiyo ililenga kuzifikia kaya zenye mazingira magumu na kutoa mahitaji mbalimbali ikiwepo chakula ,mavazi na ujenzi wa makazi.

 

Dkt. Tulia  amesema hayo jana  Julai 12 , mwaka huu na kwamba  pamoja na kuihudumia  mahitaji muhimu, pia amechukua jukumu la kuwasomesha watoto wote wa familia hiyo, akiwemo kijana Nature  aliyehitimu kidato cha nne na kupata ufaulu wa daraja la kwanza la alama 13 na kushindwa kuanza masomo ya kidato cha tano kutokana na ukata wa fedha.

 


Kwa upande wake, kijana Nature Wilson,  ameeleza namna alivyopitia ugumu katika safari yake ya masomo ikiwa ni pamoja na kukata tamaa ya kuendea kidato cha tano baada ya familia kukosa fedha.

 

"Tunaishi maisha magumu kuna wakati tunalala bila kupata chakula,lakini tulikuwa tunamuomba Mungu ambaye amemleta Spika wa Bunge  Dkt Tulia kutufuta machozi na magumu tunayopitia," amesema

 

Naye Bibi familia hiyo,  Lusia Kapangala(65)  amemshukuru Dkt. Tulia pamoja na wananchi kwa kuwa msaada kwao katika kipindi chote.

 

#KhomeinTvUpdates 

 

✍️Mwandishi wetu-Mbeya

 

PIA USIACHE KU SUBSCRIBE

CHANEL YETU Khomein TV

YOUTUBE UWE WA KWANZA 

KUFIKIWA NA HABARI ZETU

 

Follow Insta & Threads @khomeintv_

Tufollow pia kwenye X (Twitter), TikTok

@khomeintv na Facebook Khomein Tv

Post a Comment

0 Comments