Serikali imeendelea kuchukua hatua madhubuti kutokomeza tatizo la matumizi mabaya ya laini za simu, ikiwa ni pamoja na laini za TTCL, zinazotumika katika utapeli.
Hayo yamesemwa Februari 11, 2025 Bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Marypriscar Mahundi alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Sikonge, Joseph Kakunda.
Naibu Waziri Mahundi, amesema hatua zinazochukuliwa ni pamoja na usajili wa laini kwa alama za vidole ili kuhakikisha kila laini inahusiana moja kwa moja na mmiliki wake halali.
Aidha, ameongeza kuwa Serikali kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeanzisha mifumo ya kufuatilia na kufungia laini zinazotumika kwa uhalifu.
Vilevile, amesema elimu kwa umma inaendelea kutolewa kuhusu namna ya kutambua na kuripoti matukio ya utapeli kupitia namba maalum 15040.
Pia, amesema Serikali inashirikiana na watoa huduma za mawasiliano, wakiwemo TTCL, ili kuhakikisha laini zinazotumika kwa ulaghai zinadhibitiwa mara moja.
✍️Mwandishi wetu
PIA USIACHE KU SUBSCRIBE
CHANEL YETU Khomein TV
YOUTUBE UWE WA KWANZA
KUFIKIWA NA HABARI ZETU
Follow Insta & Threads @khomeintv_
Tufollow pia kwenye X (Twitter), TikTok
@khomeintv na Facebook Khomein Tv
0 Comments