Daktari Bingwa wa magonjwa ya watoto wa Hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya (MZRH), Dkt. Angela Leonard amekabidhi mashine mbili za kutoa dawa hususani kwa wenye matatizo ya kupumua katika Hosptali ya Rufaa Kanda ya Mbeya (MZRH).
Dkt Angela amekabidhi mashine hiyo jana Februari 11,2025 kwa Mkurugenzi mtendaji wa Hosptali hiyo Dkt. Godlove Mbwanji ikiwa ni sehemu ya shukrani kwa hospitali na watumishi wakati wa kutekeleza majukumu yake.
Amesema amewiwa kuchangia mashine kama sehemu ya kuboresha utoaji wa huduma kwa watoto walio na changamoto mbalimbali.
Mkurugenzi mtendaji wa Hosptali ya Kanda Dkt. Godlove Mbwanji, ameshukuru kwa mchango mkubwa ambao utasaidia kutoa huduma bora kwa watoto wanaokabiliwa na changamoto ya mfumo wa kupumua.
"Mashine hizi muhimu katika hospitali yetu zitatumika kutoa huduma bora za matibabu kwa watoto wenye changamoto mbalimbali wakiwepo wanaosumbuliwa na magonjwa ya mfumo wa upumuaji na mengine .”
Dkt. Mbwanji, ameomba na wadau wengine kuwa na tabia ya kujitoa kuchangia huduma za afya kama sehemu ya shukrani ili kupata baraka ya mafanikio kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
Awali, Dkt. Angela, amesema ameamua kutoa mashine ili kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuboresha sekta ya afya nchini.
“Naamini kuwa kila mtoto ana haki ya kupata matibabu bora mashine zitarahisisha mchakato wa matibabu na kuokoa maisha ya watoto wengi, "amesema.
✍️Mwandishi wetu-Mbeya
PIA USIACHE KU SUBSCRIBE
CHANEL YETU Khomein TV
YOUTUBE UWE WA KWANZA
KUFIKIWA NA HABARI ZETU
Follow Insta & Threads @khomeintv_
Tufollow pia kwenye X (Twitter), TikTok
@khomeintv na Facebook Khomein Tv
0 Comments