Serikali ya Awamu ya Sita kupitia Wizara ya Nishati imedhamiria kuing'arisha nchi kwa kuwawekea umeme wa uhakika na wananchi katika maeneo yote nchini.
Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri wa Nishati Judith Kapinga,
Februari 03, 2025, bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la la Mbunge wa Lushoto Shabani Shekilindi aliyetaka kufahamu ni lini Serikali itaondoa changamoto ya kukatika umeme katika Wilaya ya Lushoto kwa kuweka suluhisho la kudumu.
Kapinga amesema azma ya Serikali ni kuhakikisha wananchi wanapata umeme wa uhakika na unaotabirika kwa ajili ya shughuli za kijamii na kimaendeleo.
"Tutafuatilia kwa hii wiki moja kufahamu ni nini changamoto ya kukatika kwa umeme Wilaya ya Lushoto, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge iwapo kuna matengenezo tutahakikisha yanakamilika kwa haraka." Amesisitiza Kapinga
Akijibu swali Mbunge wa Nkasi Kusini, Vicent Mbogo aliyetaka kufahamu uwepo wa nishati ya umeme katika Kijiji cha Msamba-Masokolo, Lyapinda, Izinga na Lyele na katika Vitongoji vya Kisenga na Lupata, Kapinga amesema Wilaya ya Nkasi ina jumla ya vijiji 90 ambapo vyote vimepatiwa huduma ya umeme vikiwemo vijiji vya Lyele na Lyapinda.
Aidha, amesema Kitongoji cha Lupata kilichopo katika Kijiji cha Lyapinda kitapata umeme kupitia mradi wa Vitongoji 15 vya Mbunge utakaotekelezwa na Mkandarasi aitwae M/s STEG International Services Ltd ambaye ameshakamilisha hatua za upimaji na usanifu.
Ameongeza kuwa, uhakiki wa Kitongoji cha Kisenga umekamilika na Kitongoji hicho kitapatiwa umeme kupitia mradi wa vitongoji (HEP IIB).
✍️ Mwandishi wetu
PIA USIACHE KU SUBSCRIBE
CHANEL YETU Khomein TV
YOUTUBE UWE WA KWANZA
KUFIKIWA NA HABARI ZETU
Follow Insta & Threads @khomeintv_
Tufollow pia kwenye X (Twitter), TikTok
@khomeintv na Facebook Khomein Tv
0 Comments