SERIKALI YAJIVUNIA MATUNDA YA WANAWAKE WAPAMBANAJI

 

Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Nishati,  Neema Mbuja imesema, kile ambacho wanawake walikipambania katika majukwaa mbalimbali ikiwemo ya Kimataifa ili kuwa na haki, usawa na uwezeshaji kwa wanawake matunda yake yanaonekana hivi sasa.

 

Hayo yamehabarishwa na Mbuja wakati akieleza safari ya mwanamke katika kudai haki, usawa na uwezeshaji kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo nchini Kitaifa yatafanyika mkoani Arusha.

 

"Wanawake wengi walipambana kuhakikisha kunakuwepo na usawa wa kijinsia, usawa wa utendaji kazi na ushiriki katika nafasi mbalimbali za uongozi na tangu kufanyika kwa Mkutano wa Beijing  mwaka 1995 mambo yote ya usawa kwa sasa yanaonekana kwa vitendo." Amesema Mbuja

 

Ameeleza kuwa Serikali   imekuwa kinara katika kuhakikisha haki kwa mwanamke inapatikana.

 

Ameongeza kuwa, Wizara ya Nishati inajivunia kwa uwepo wa wanawake katika nafasi mbalimbali za uongozi.

 

#KhomeinTvUpdates 

 

✍️ Mwandishi wetu

 

PIA USIACHE KU SUBSCRIBE

CHANEL YETU Khomein TV

YOUTUBE UWE WA KWANZA 

KUFIKIWA NA HABARI ZETU

 

Follow Insta @khomeintv_

 

Tufollow pia kwenye X (Twitter), TikTok

@khomeintv na Facebook Khomein Tv

Post a Comment

0 Comments