UWANJA WA KISASA WA SAMIA KIELELEZO CHA MAENDELEO YA MICHEZO TANZANIA

 

Ujenzi wa Uwanja wa Mpira wa Kisasa unaoendelea jijini Arusha, maarufu kama Uwanja wa Samia Suluhu Hassan, umefikia asilimia 51. Uwanja huu unajengwa katika eneo la Olomoti, ambapo kazi ya umwagaji wa zege kwenye muundo mkuu wa jengo imeanza, ikikadiriwa kufikia mita za ujazo 50,000.

 

Mradi huu mkubwa unatarajiwa kukamilika ifikapo Julai 24, 2026, ukiwa ni sehemu ya maandalizi ya mashindano ya AFCON 2027. Ambapo Tanzania ni mwenyeji mwenza sambamba na Kenya na Uganda.

 

Tanzania inapiga hatua kuhakikisha inakuwa na miundombinu ya kisasa ya michezo. Uwanja huo mpya utakuwa na uwezo wa kuchukua watazamaji 30,000, na ni moja kati ya viwanja vitakavyotumika katika mashindano hayo ya kimataifa. Kukamilika kwake si tu kutakuza michezo, bali pia kutachangia maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika mkoa wa Arusha na Taifa kwa ujumla.

 

#KhomeinTvUpdates 

 

✍️Mwandishi wetu

 

PIA USIACHE KU SUBSCRIBE

CHANEL YETU Khomein TV

YOUTUBE UWE WA KWANZA 

KUFIKIWA NA HABARI ZETU

 

Follow Insta & Threads @khomeintv_

Tufollow pia kwenye X (Twitter), TikTok

@khomeintv na Facebook Khomein Tv

Post a Comment

0 Comments